ZLATAN IBRAHIMOVIC HATARINI KUTOCHEZA TENA MSIMU HUU



ZLATAN IBRAHIMOVIC HATARINI KUTOCHEZA TENA MSIMU HUU

Zlatan Ibrahimovic ameumia vibaya goti ukingoni kabisa mwa dakika 90 za mchezo wa Europa League Alhamisi usiku dhidi ya Anderlecht.

Mshambuliaji huyo wa Manchester United aliruka juu na kutua vibaya mguu wake wa kulia na kulazimika kutolewa  huku nafasi yake ikichukuliwa na Anthony Martial. 


Kuna mashaka makubwa iwapo nyota huyo wa miaka 35 ataweza kucheza tena msimu huu.


Comments