Fifa Yaibeba Serengeti Boys


Fifa Yaibeba Serengeti Boys
Timu ya Taifa ya vijana wa chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) imepata nafuu zaidi kuelekea kufuzu mashindano ya Kombe la Dunia nchini India baada ya hatua ya Shirikisho la Kandanda Duniani (Fifa) kuifungia Mali kushiriki katika mashindano ya fainali za Afrika kwa Vijana nchini Gabon.

Afisa Habari wa TFF, Alfred Lucas amesema kuwa tayari Shirikisho la Kandanda la Afrika (Caf) limeindoa Mali imeitangaza nchi ya Ethiopia kuungana na Tanzania, Angola na Niger katika kundi B la mashindano hayo.

Lucas amesema kuwa Mali ndiyo mabingwa watetezi wa mashindano hayo na walikuwa  na kikosi chenye wachezaji nyota ambao kwa namna moja au nyingine wangeisumbua sana Serengeti Boys.

Wakati huo huo: timu ya Serengeti Boys itacheza mechi tatu za kirafiki nchini Morocco ikiwa ni sehemu ya maandalizi kabla ya kwenda Cameroon na Gabon.

Timu hiyo itacheze mechi mbili dhidi ya Gabon siku ya Aprili 22 na 25 na baadaye itacheza mechi dhidi ya Morocco  Aprili 28 na baadaye kusafiri kwenda  Cameroon kucheza mechi mbili dhidi ya Cameroon Mei 3 na Mei 6 na seku inayofuata timu itasafiri kwenda Gabon.




Comments