KOCHA wa Real Madrid, Zinedine Zidane              amesema kuwa anahitaji kuwapa muda mwingi zaidi wa kucheza              nyota wake Isco na Alvaro Morata, baada ya kuisaidia timu              hiyo kutoka nyuma na kisha wakafanikiwa kuondoka na ushindi              dhidi ya Villareal katika mchezo wa Ligi Kuu ya Hispania "La              Liga" uliopigwa juzi.
        Katika mchezo huo uliopigwa katika uwanja              wa Estadio de la Ceramica, vijana hao wa Zidane walilazimika              kutoka nyuma kwa mabao mawili na kisha wakaondoka kifua              mbele kwa ushindi wa 3-2, yaliyofungwa katika dakika ya 26              za mwisho.
        Isco alitokea benchi wakati matokeo              yakiwa 2-0 na akatoa mchango mkubwa uliosaidia kupatikana              mabao mawili wakati Morata aliingia uwanjani wakati timu              hizo zikiwa 2-2 na kisha akafunga bao la ushindi wakati              zikiwa zimebaki dakika saba.
        Msimu huu Isco na Morata wamechezeshwa              mechi 11 na saba za Ligi na kwa matokeo hayo ya juzi, Zidane              amesema kuwa kuna kitu kinatakiwa kufanyiwa mabadiliko.
        "Hakuna shaka kwamba Isco na Morata              wanahitaji muda zaidi wa kucheza," kocha huyo wa Real Madrid              aliwaambia waandishi wa habari.
        "Wamefanya kazi nzuri na kubadili mchezo              kwa upande wetu. Nimebaini wanahitajika katika kisi chote,"              aliongeza.
        
Comments
Post a Comment