KOCHA            Sir Alex Ferguson ndiyo nembo iliyoko nyuma ya mafanikio ya            Manchester United kuanzia mwaka 1986 hadi 2013 aliwapa karibia            kila kombe kuanzia Uingereza Ulaya na Dunia nzima.
        Tangu baada ya Ferguson kuondoka timu              hiyo imekuwa ikiyumba huku makocha wawili waliomfuata David              Moyes na Luis Van Gaal wakishindwa kuwapa kile wanachotaka,              huku kocha wao wa sasa Jose Mourinho kidogo akianza              kuwafuraisha.
        Tayari mashabiki wa Manchester United              dunia nzima walianza kupiga kelele wakitaka Ferguson arudi              kutetea Jahazi lao linaonekana kuzama kabla ya Morinho              kuanza kuwainua.
        Lakini sasa kiu ya mashabiki wengi wa              Manchester United ya kumuona Ferguson akiwa kwenye benchi la              Old Traffold kama kocha inaelekea kutimia, Ferguson atarudi              kama kocha wa United Juni 4, mwaka huu.
        Ferguson ambaye hadi anastaafu alishawapa              United jumla ya makombe 26, atakuwepo kwenye mchezo maalum              kwa ajili ya kiungo wa Manchester United, Michael Carrick.
        Ferguson katika mchezo huo atakuwa kocha              wa wachezaji wa zamani wa Mancherster United.
        Ferguson atakuwa kocha wa kikosi cha              wachezaji wa zamani wa United ambao watacheza na timu ya              Carric.
        Pengine hii itawavutia sana washabiki wa              Manchester United, kwani toka Ferguson  atangaze kuustafu              hawajawai tena kumuona akisimama nje ya uwanja kama kocha. 
        
Comments
Post a Comment