KOCHA wa Manchester United, Jose Mourinho              amewashutumu wachezaji wa Leicester City kwa kuwa na              ubinafsi wa kumsaliti aliyekuwa kocha wao, Claudio Ranieri.
        Mreno huyo alivaa kofia yenye nembo za              "CR" akimuunga mkono Ranieri kabla ya kuwashutumu wachezaji              hao ambao wengi wao walisaini mikataba mipya baada ya              kushinda taji la Ligi.
        Mourinho alifutwa kazi katika mazingira              kama hayo msimu uliopita kufuatia mgomo wa wachezaji, lakini              akasema kuwa kisa alichofanyiwa kilikuwa kidogo sana              ikilinganishwa na vile Ranierio alivyofanyiwa.
        "Nadhani msimu huu ulianza na ubinafsi              mwingi wachezaji wakitaka kupewa mikataba mipya." 
        "Watu wakifikiria fedha zaidi wengine              wakiamua kuondoka bila kujali ni nani aliyewafanya kufika              walivyo," alisema Mourinho.
        Mourinho aliongeza kusema kwamba              wachezaji wengi mara zote wamekuwa wabinafsi kiasi kwamba              wanachangia makocha kuonekana sio watu wa muhimu wakati              kumbe ndio chachu ya mafanikio ya klabu.
        "Ukiangalia kilichonitokea mimi pale              Chelsea kinaweza kulingana kabisa na kile kilichomtokea              Ranieri, kwasababu haiwezekani kocha awape ubingwa leo hii              mumuone hafai."
        "Wachezaji wamechangia kwa kiasi kikubwa              sana kuhakikisha Ranieri anatupiwa virago nah ii ni tabia ya              kawaida sana katika klabu nyingi za Ulaya, kwa hakika kabisa              hali hii haikubaliki."
        Ranieri baada ya kuipandisha Ligi Kuu              Leicester aliifanikisha kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa mara              ya kwanza na kuiwezesha kushiriki michuano ya Ligi ya              Mabingwa kwa mara ya kwanza msimu huu.
        
Comments
Post a Comment