Badri Har raia wa Morocco alijipatia umaarufu sana baada ya kuonekana na ukaribu usio wa kawaida na Cristiano Ronaldo.Mambo mengi yalisemwa kuhisu wawili hao lakini picha ambayo Badri alionekana amempakata Ronaldo ilizua mijadala mingi mitandaoni wengine wakimhusisha Ronaldo na ushoga.
Sasa Badri amehukumiwa kwenda jela miqka miwili          baada ya kufanya mashambulio kwa watu.Badri mwenye miaka 32          amefanya matukio hayo nchini Uholanzi japokuwa kesi yake ilikuwa          ikiendeshwa Morocco.Na sasa kesi hiyo imerudishwa tena mjini          Amsterdam ili kujaribu kuharakisha hukumu yake.Na sasa mahakama          imemhukumu Badri kwenda kukaa jela miaka miwili.
        Mwaka 2012 Badri anatuhumiwa kuhusika katika tukio          la kupigana na kumshambulia mtu mjini Amsterdam.Lakini baada ya          kufanya tukio hilo Badri tena kwa kutumia chupa alimshambulia          mtu katika ukumbi wa starehe unaotajwa kumilikiwa na mtu aitwaye          Jimmy Woo.
        Hii sio mara ya kwanza kwa Badri kwenda jela kwani          mwaka 2015 alienda jela kwa kosa la namna hii hii.Na kwa kosa          hili inaonekana Badri anaweza kukaa jela kwa muda mrefu          zaidi.Hii inamaanisha Badri hatamuona kwa kipindi kirefu rafiki          yake Cristiano Ronaldo.
        Mwaka 2015 jarida la kiarabu liitwalo Aljabar Al          Yaum lilisema Cristiano Ronaldo alitenga kiasi cha £ 2400 kwa          ajili ya kuchukua chumba cha hotel.Chumba hicho ilisemekana ni          katika hotel iitwayo The Pearl Marakech na Ronaldo alitaka          kukitumia yeye na Badri.Ripoti zingine zilisema mwaka 2015          Ronaldo alikuwa akitumia ndege yake binafsi aina ya Gulfsteem          G200 kusafiri kwenda Morocco kumuona Badri mara 4 kwa mwezi.
        Japokuwa kumeendelea kuwa na tetesi zinazomhusisha          Ronaldo na ushoga lakinu mpiga soka huyo yeye hajawahi kuongea          lolote.Lakini Ronaldo amendelea tu kutoka na walimbwende kwani          baada ya kuachana na mrembo Irna Shayk sasa Ronaldo yuko na          mlimbwendwe mwingine Georgina Rodriguez.
        
Comments
Post a Comment