Siku za Wayne Rooney kuwa United inaonekana zinahesabika.Ujio wa Mhiktaryan,Zlatan Ibdahimovich na Athony Martial unaiweka nafasi ya Rooney katika timu hiyo kuwa mashakani.Umri wa Rooney umeenda na kiwango kimeshuka na hii inamfanya kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza cha Man United.
Rooney ameshawahi sana kuhusishwa                    kuondoka Man United,haijaanza leo kwa Rooney                    kuhusishwa na uhamisho wa kuondoka United,kama                    umfuatiliaji mzuri wa masuala haya utakumbuka msimu wa                    mwisho wa Alex Ferguson Wayne Rooney alihusishwa na                    uhamisho wa kwenda Chelsea japo jambo hilo                    halikutokea.
                  Lakini sasa tetesi za Rooney kuondoka                    Man United zimepamba moto sana.Wakati wa dirisha dogo                    la usajili la January kuliibuka tetesi za Wayne                    kuhamia ligi ya China.Japokuwa klabu ambayo ilikuwa                    ikihitaji huduma ya Wayne Rooney haikutajwa kwa                    kipindi hicho ila ilikuwa ni wazi kwamba Wayne                    angevutwa China kutokana na nguvh kubwa ya kifedha ya                    timu za nchi hiyo.
                  Tianjin Quanjian timu inayonolewa na                    nahodha wa zamani wa Italia Fabio Cannavaro imekiri                    kuwahi kufanya na Rooney mazungumzo.Cannavaro amekiri                    walimuhitaji Rooney japokuwa hafiti katika staili yake                    ya uchezaji ila walijaribu kutaka kumsajili Wayne                    Rooney.
                  Tianjin Quanjian bado wanapewa nafasi                    kubwa kumnunua Rooney,japokuwa wanasema katika mipango                    yao ya usajili jina la mshambuliaji wa Borussia                    Dortmund Pierre Aubemayang ndio liko juu.Tianjin pia                    wako na mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Fiorentina                    Nikola Kalinic ili kuweza kuimarisha safu yao ya                    ushambuliaji.
                  Kocha wa Man United Jose Mourinho                    amezidi kukuza tetesi za Rooney kuondoka baada ya                    kukataa kueleza kuhusu usajili wa Rooney.Mourinho                    aliwaambia waandishi wa habari kama wanataka kujua                    kuhusu masuala ya Rooney kuondoka United baasi                    wakamuulize Rooney mwenyewe.Kauli hiyo ya Mourinho                    imetafsiriwa kama kukosa uhakika kubaki na Rooney                    msimu ujao.
                  Dirisha la usajili nchini China linaisha                    siku ya Jumanne ijayo.Wakala wa Wayne Rooney aitwaje                    Paul Steford amesafiri hadi China kujaribu kufanya                    mazungumzo na baadhi ya timu ikiwemo Tianjin.Tayari                    Wachina wapo tayari kumlipa Rooney £600,000 kwa wiki                    kiasi ambacho ni mara mbili ya mshahara wa sasa                    anaopokea.
                
Comments
Post a Comment