Asamoah Gyan mchezaji wa timu ya taifa ya Ghana ambae kwa sasa anakipiga Dubai katika timu ya Al Ahli ambapo yupo kwa mkopo akitokea Shanghai SIPG ya China ni kati ya wachezaji mabishoo sana.Gyan kama kijana nje ya soka huwa anapendelea sana mambo ya mitindo na muziki na hata muonekano wake huwa uko kisanii sanii.
Sasa ubishoo wa Gyan unaelekea kumtokea puani huko          Uarabuni.Waarabu wana sheria zao sana katika nchi zao na moja ya          sheria zao ni kuhusu unyoaji wa nywele.Gyan amekutwa na hatia          katika unyoaji wake wa nywele na sasa itamlazimu kukaa nje ya          uwanja hadi hadi hapo atakapobadili staili yake ya nywele.
        Sio Gyan tu aliyekutwa na kadhia hiyo kwani kuna          wachezaji wengine 40 ambao nao wamekumbwa na suala kama          hili.Sheria za waarabu nchini humo zinakataza unyoaji wa style          ya kunyoa pembeni ya kichwa na kuacha tu nywele juu ya kichwa          almaarufu kama kiduku,mtindo ambao Gyan amekuwa akiutumia sana.
        Mwaka 2012 golikipa wa timu moja huko Duba aitwaye          Waleed Abdullah alitolewa nje kabla ya mechi kuanza akitakiwa          akanyoe vizuri nywele zake.Gyan alionekana katika mashindano ya          kombe la mataifa Afrika akiwa kanyoa kiduku chake huku pembeni          akiwa amechonga herufi ya W.Hii ni kama majanga yanaendelea kwa          Gyan baada ya kushuhudia timu yake ya taifa ikiondolewa katika          mashindano ya mataifa Afrika kwa kipigo cha bao mbili toka          Cameroon.
        
Comments
Post a Comment