Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Arsenal, Thierry Henry          amewaambia mashabiki wa Arsenal kuwa kocha wa klabu hiyo Arsene          Wenger hatakiwi kuondoka klabuni hapo, lakini amekiri kuwa kocha          huyo ana kazi ya ziada kuibadili klabu hiyo kuwa na kariba ya          kugombea ligi kuu ya Uingereza.
          Imekuwa miaka 13 tangu mzee Wenger atwae taji la ligi kuu ya          Uingereza alilolitwaa mara tatu tangu ajiunge na klabu hiyo          mwaka 1996. Henry aliyejiunga na Arsenal chini ya Arsene Wenger          amekiri kuwa kazi ni kubwa mbele lakini Wenger sio wa kuondoka.
          "Binafsi, nadhani Arsene hatakiwi kuondoka," Henry, ambaye          alipewa nafasi ya kikosi cha kwanza na Wenger katika klabu ya          Monaco akiwa na umri wa 17, aliiambia RMC. "Kuhusu kubadili          mbinu na aina ya uchezaji? Sina uhakika kama yupo tayari. Lakini          kazi anayotakiwa kufanya sasa hivi inahusisha mambo mengi kama          suala la kiakili.
          "Mbinu zinasaidia, lakini kile nilichokiona [walipopoteza 3-1          dhidi ya Chelsea], it's lilikuwa tatizo la kiakili/kifikra. Ni          kitu nilichokiona kwa muda mrefu kiasi sasa. Na hapo ndipo ugumu          wa kazi wa Wenger ilipo na inapoendelea kuwa ngumu zaidi, kwa          sababu ni tatizo lililo kifikra zaidi. Sio rahisi kulitatua.
          "Arsenal hawajashinda ubingwa kwa miaka 12, na unaweza kuamini          kuwa hawawezi kushinda kwa msimu huu. Nahisi kuna ubora kwenye          kikosi chao. Inajitosheleza kushinda ubingwa? Mwanzo wa msimu,          ulikuwa ukitizama Chelsea na Arsenal kwenye karatasi, hapakuwa          na tofauti kubwa, hivyo inawezekana.
Comments
Post a Comment