Miamba wa soka wa Hispania Fc          Barcelona wameanza vibaya hatua ya kumi na sita bora baada ya          kukubali kichapo cha mabao 4-0 ugenini dhidi ya Psg ya Ufaransa.
        Angel di Maria alianza kuwaandika          Pgs goli kwa mpira wa adhabu uliokwenda moja kwa moja nyavuni,          katika dakika ya 40 mshambuliaji mpya wa Wafaransa hao Julian          Draxler akaongeza bao la pili.
        Dakika ya 55 Angel di Maria tena          akawachapa Barca bao la tatu, kabla ya Edinson Cavan kuhitmisha          shughuli kwa bao la nne .
        Katika mchezo mwingine Benfica ya          Ureno wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Borrrusia Dotmund          ya Ujeruman kwa bao la Konstantinos Mitroglo.
        Ligi hiyo itaendlea tena leo kwa          michezo miwili Bayern Munich wakiwalika Arsenal nao Real Madrid          wakiwa wenyeji wa Napoli.
        
Comments
Post a Comment