Wakati klabu ya Liverpool ikiwa katika fomu mbovu kutokana na          kutokupata ushindi katika mwezi januari kwenye ligi kuu ya          Uingereza, Taarifa zinasema klabu hiyo ilikuwa inunuliwe na          tajiri namba moja duniani na mmiliki wa Microsoft Bill Gates          pamoja na mmiliki wa mabingwa wa kihistoria wa Super Bowl, New          England Patriots bwana Robert Kraft kipindi ambacho waliokuwa          wamiliki wa klabu hiyo Tom Hicks na George Gillett walipoamua          kuiuza.
          Taarifa zimetolewa na nyaraka zilizopatikana katika mahakama          kutokana na taarifa za ushindani wa kisheria kati ya kampuni          inayofahamika kama Mill Financial and Gillett na ile ya Royal          Bank of Scotland. Hicks na Gillett walikubali kuiuza Liverpool          mwezi April 2010 baada ya kushindwa marejesho ya fedha          walizokopa wakati wanainunua klabu hiyo mwaka 2007.
          Barclays Capital walipewa kazi ya kutafuta wanunuzi, na nyaraka          kutoka kwenye kanda ya kiuchumi katika mahakama kuu ya New York          County Supreme Court zinaonyesha kuwa Bill Gates, mwanzilishi wa          Microsoft, alifuatwa katika yangazo la wahitaji wa kuinunua          klabu hiyo.
          Martin Broughton, ambaye alikuwa mwenyekiti wa Liverpool kipindi          hicho, aliulizwa kama kulikuwa na ukweli juu ya kufuatwa kwa          Bill Gates na Bob Kraft, akajibu "ni kweli kabisa"
          Broughton aliulizwa pia kama alikuwa anafahamu kama Barclays          Capital walikuwa wanafuatilia jitihada zilizokuwa zinafanywa na          wawekezaji wa Hong Kong, Norway.
          Alijibu kwa kusema, utafutaji wa wawekezaji wapya ulifanyika          katika kila bara na ulihusu kuwasiliana na watu tofauti duniani          kote.  Bill Gates hakujibu au kuitikia wito lakini Kraft alisita          katika kuinunua klabu hiyo huku pia akiwa alikataa ofa ya David          Moores mwaka 2005.
          New England Sports Ventures, wanaofahamika kama Fenway Sports          Group, hatimae waliinunua Liverpool kwa dau la £300 million          mwezi October 2010, huku Hicks na Gillett wakisema dili lile          lilikuwa wizi wa mchana.
Comments
Post a Comment