MLINDA mlango              Thibaut Courtois amezitolea nje timu mbili za La Liga ambazo              zilikuwa katika orodha ya kumwania katika usajili wa dirisha              la Januari mwakani.
        Akikanusha mlinda              mlango huyo alisema pamoja na kuakiwa na timu za Atletico na              Real Madrid msimamo wake ni kutotaka kurejea kukipiga katika              Ligi hiyo ya Hispania.
        Kutokana na hilo              Thibaut amesisitiza dhamira yake ya kutaka kubakia ndani ya              kikosi cha matajiri wa Darajani Chelsea.
        Courtois mwenye              umri wa miaka 24 aliitumikia kwa mkopo Atltico Madrid na              kuisaidia kushinda mataji ya Winning La Liga ikiwemo ubingwa              wa Copa del Rey na ubingwa wa Ligi ya Ulaya.
        Pia aliisaidia              Atletico kufikia fainali ya Ligi ya Mabingwa ya Ulaya mnamo              mwaka 2014.
        Akinukuliwa              mlinda mlango huyo amesema kwa sasa anajivunia hatua ya kuaminika kama nambari moja ndani ya            Chelsea hatua inayompa faraja kubwa.
        "Ninachoweza              kusema ni kwamba sijazungumza na timu yoyote kati ya              Atletico ama Real Madrid hivyo taarifa zote za uvumi ni              uzushi mkubwa."
        "Nina jisikia              furaha kuwepo hapa Chelsea nina heshima kubwa hapa hivyo              sitarajii kuondoka kwa sasa."
        
Comments
Post a Comment