NI wazi mashabiki              wa Chelsea wamesahau wakati mshambuliaji wao kinara wa mabao              Ligi Kuu England kwa sasa, Diego Costa alipoonyesha dhamira              kurudi Atletico Madrid.
        Lakini kitendo              cha Costa kupiga picha akiwa na kocha wa Atletico, Diego              Simeone wakifurahia chakula cha jioni, kimewashitua.
        Costa kwa sasa              yuko Hispania kwa ajili ya kuchezea timu ya taifa mechi ya              kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia dhidi ya Macedonia.
        Kuwepo kwake              nyumbani Hispania kulimpa fursa ya kukutana na marafiki na              kocha wake wa zamani.
        Costa alituma              picha kwenye mtandao wa kijamii akiwa na kocha wake wa              zamani na kuandika: "Furaha kubwa kuungana tena."
        Zaidi ya watu              35,000 waliipenda picha hiyo, huku wengine 500 wakiandika              ujumbe.
        Baadhi ya watu              waliotuma ujumbe kuhusiana na picha hiyo waliwaponda              mashabiki wa Chelsea ambao miezi mitatu iliyopita walisikika              kauli ya mchezaji huyo kutaka kuondoka. 
        
Comments
Post a Comment