MANCHESTER UNITED YAFUFUKA KWA SWANSEA ...Zlatan Ibrahimovic atupia mbili, Pobga wee wacha tu, Rooney usipime
MANCHESTER UNITED            imecharuka na kuvuna ushindi wa bao 3-1 dhidi ya Swansea            katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
        Paul Pogba alifunga            bao tamu dakika ya 15 katika 'muvu' ambayo aliianzisha            mwenyewe kabla ya kuachia mkwaju wa mbali uliokwenda moja kwa            moja wavuni.
        Ilikuwa siku njema            kwa Zlatan Ibrahimovic ambaye alifunga mara mbili dakika ya 21            na 33 na kumaliza ukame wa muda mrefu wa kutoka uwanjani bila            goli katika mechi za Premier League.
        Bao pekee la            Swansea lilifungwa na Mike van der Hoorn dakika ya 69 huku            kocha wa Manchester United akiutazamia mchezo huo jukwaani            kufutia kufungiwa kukaa kwenye benchi kwa mechi moja.
        Nahodha Wayne            Rooney amerejeshwa kwenye kikosi cha kwanza na kuwa nyota wa            mchezo huku msaidizi wake Michael Carrick naye akianzishwa na            kutakata vilivyo.
        SWANSEA (4-4-2):            Fabianski 5.5; Rangel 5, Van der Hoorn 6, Mawson 6, Kingsley            5.5; Routledge 4 (Barrow 46mins, 5.5), Britton 5 (Fer 70, 5),            Ki 5, Sigurdsson 5.5;  Borja Baston 5, Llorente 4 (Montero 46,            5)
        MANCHESTER UNITED            (4-3-3): De Gea 6; Young 6, Jones 6.5, Rojo 6.5, Darmian 6;            Carrick 7, Fellaini 6.5, Pogba 6.5 (Fosu-Mensah 90+4); Mata            6.5 (Lingard 82), Rooney 8 (Schneiderlin 89), Ibrahimovic 7.5
        Zlatan Ibrahimovic              akishangilia kwa staili ya Kung Fu 
        Paul Pogba akiifungia              United bao la kwanza
        
Comments
Post a Comment