HATMA ya Luke Shaw            na Chris Smalling ndani ya Manchester            United iko mashakani baada ya kocha            Jose Mourinho kusema baadhi ya wachezaji wake hawana uwezo wa            kujitoa muhanga  na kucheza wakiwa na maumivu.  
        Mabeki hao wa            England walikosekana katika mchezo wa Premier League wa            ushindi wa 3-1 dhidi Swansea Jumapili iliyopita baada ya            kumwambia Mourinho kuwa hawawezi kucheza. 
        Mourinho naye            akaanzisha mashambulizi ya kiaina wakati akifanya mageuzi            kwenye safu yake ya ulinzi kwa kusema: "Tuna wachezaji wenye            matatizo."
        Kocha huyo            akawasilisha ujumbe huo hadi kwenye vyumba vya kubadilishia            nguo mbele ya wachezaji na kutoa taswira kuwa wawili hao            hawana nafasi tena Manchester United. 
        "Luke Shaw            aliniambia kuwa hayuko katika hali nzuri kuweza kucheza dhidi            ya Swansea, hivyo tulipaswa kujenga upya safu yetu ya ulinzi.            Kuna tofauti kubwa sana kati ya mchezaji ambaye yupo tayari            kucheza kwa gharama yoyote na mchezaji anayehofia kuingia            uwanjani kwasababu tu ana maumivu madogo," alisema Mourinho.
        Kocha huyo            alimpongeza  Smalling mwenye umri wa miaka 26 kwa kucheza            mchezo wa kipigo cha 4-0 dhidi ya Chelsea Oktoba 23 huku akiwa            amechomwa sindano za kuzuia maumivu lakini katika mechi ya            Swansea Mourinho akasema: "Smalling hajisikii kama anaweza            kucheza kwa asilimia 100 kwa maumivu aliyonayo."
        Kocha Manchester United               Jose Mourinho akiwa jukwaani kwenye mchezo dhidi ya              Swansea 
        Luke Shaw (pichani) na              Chris Smalling wamelikoroga kwa Mourinho
        Smalling (kulia)              hakucheza dhidi ya Swansea
        
Comments
Post a Comment