STAA Daniel              Sturridge anasemekana kuwa yuko tayari kuitema klabu yake ya              Liverpool kwa kile kinachodaiwa ni kukerwa na kuwekwa              benchi.
        Kwa mujibu wa              gazeti la Daily Mirror, straika huyo wa timu ya taifa ya              England hana raha kwenye klabu hiyo ya Anfield na huenda              akaondoka kwenye klabu hiyo ya Merseyside wakati wa usajili              wa majira ya baridi yajayo.
        Kutokana na hali              hiyo, klabu mbalimbali zimeshaanza kupiga jaramba baada ya              kubaini kuwa Sturridge hayuko katika mipango ya kocha wake              Jurgen Klopp.
        
Comments
Post a Comment