Jose          Mourinho na Wenger leo wanaziongoza timu zao kucheza mechi          nyingine kwenye ligi ya England. Sasa kutokana na historia ya          ugomvi wao wa maneno hizi hapa ni Quote ambazo zimetokana na          maneno kati yao.
          2015:
          Jose Mourihno : "Ninaogopa kufeli, Yeye (Wenger)            amebobea kwenye kufeli mimi hapana. Sasa kama swala kufeli ni            kweli mimi naogopa kufeli kwasababu sifeli mara zote na wala            kufeli sio kitu changu. Lakini yeye(Wenger) ni mtaalamu wa            kufeli kwasababu miaka nane hajapata chochote cha kujivunia"
2005:
          Arsene Wenger: "Yeye(Mourihno) yupo nje ya utaratibu na            kiukweli hana adabu. Ukiwapa mafanikio watu wasiokuwa na akili            akili zinawatoka zaidi ya kuongezeka"
          2010: Wenger akizungumzia jinsi Madrid ilivyocheza kwenye UCL.
          Arsene Wenger: "Ukiangalia kwenye Tv ni njia nzuri ya            kuona kwamba hawatakiwi kufanya vile tena. Ni kitu kibaya            wamefanya kutoka kwenye club kubwa"
          2010: Morinho akamjibu
          Jose Mourihno: "Badala ya Wenger kuzungumzia Real            Madrid inabidi azungumzie Arsenal. Kupoteza kwake wa 2-0 ni            fundisho kwake kwamba historia ya watoto wadogo kwenye kikosi            chake imesha sasa hivi. Sagna, Walcott, Fabregas, Nasri, Van            Parsie sio watoto tena ni watu wazima".
          2015: Mourinho amdhihaki Wenger
          "Kuna makocha wengine kwa mara ya mwisho wameshinda taji            ni miaka 10, mimi nimeshinda mwaka mmoja uliopita. Kama kuna            kitu cha ku-prove tayari ninacho. Fikiria wengine walivyo            wakati sisi kwetu kumaliza nafasi ya nne sio lengo letu."
Comments
Post a Comment