ARSENAL            imepunguzwa kasi na Tottenham baada ya kulazimishwa sare ya            1-1 kwenye mchezo Ligi Kuu ya England.
        Harry Kane ndiye            aliyefuta matumaini ya Arsenal kukaa kileleni mwa Ligi Kuu kwa            kuifungia Tottenham bao la kusawaisha kwa mkwaju wa penalti            dakika ya 51, hiyo ikiwa ni mara yake ya nne kuitungua Arsenal            katika mechi tano zilizopita.
        Kevin Wimmer            aliizawadia Arsenal bao la kuongoza baada ya kujifunga dakika            ya 42 na kuwafanya vijana wa Wenger waende mapumziko wakiwa            mbele.
        ARSENAL XI            (4-2-3-1): Cech 6.5; Bellerin 7, Mustafi 5, Koscielny 6,            Monreal 6.5; Coquelin 6.5 (Ramsey 65mins, 5), Xhaka 7; Walcott            6 (Oxlade-Chamberlain 71, 5), Ozil 7, Iwobi 5.5 (Giroud 70,            5); Sanchez 5.5
        TOTTENHAM XI            (3-4-1-2): Lloris 7; Dier 6.5, Wimmer 5.5, Vertonghen 7;            Walker 5.5 (Trippier 80), Wanyama 7, Dembele 7.5, Rose 6.5;            Eriksen 6.5; Son 5.5 (Winks 89), Kane 6.5 (Janssen 73, 5)  
        Kane akiusukumiza mpira              wavuni kwa penalti
        Kevin Wimmer akijifunga              na kuipa Arsenal bao la kuongoza
        
Comments
Post a Comment