WACHEZAJI wawili              wa timu ya soka ya Sparta Prague wameambiwa kufanya mazoezi              na timu ya wanawake baada ya kutoa matamshi ya kiubaguzi              dhidi ya maafisa wanawake wanaosimamia mechi.
        Kipa Tomas Koubek              mwenye umri wa miaka 24, alisema kuwa: "Wanawake wanafaa              kuwa jikoni baada ya naibu refa Lucie Ratajova kushindwa              kuinua bendera kwa mchezaji ambaye alikuwa ameotea wakati wa              mechi ya siku ya Jumapili ambapo walitoka sare ya 3-3 na              Brno.
        Kiungo wa kati,              Lucas Vacha mwenye umri wa miaka 27 alichapisha picha katika              mtandao wake wa Twitter ikiwa na matamshi: "Waelekee              jikoni."
        Ofisa mkuu wa              klabu ya Sparta, Adam Kotalik aliyataja matamshi hayo kama              yasiyokubalika.
        akizungumza baada              ya mechi ya Jumapili, raia huyo wa Jamhuri ya Czech              aliongezea: "Wanawake hawafai kusimamia mechi za wanaume."
        Baadae              alichapisha picha ya mkwe na mwanawe wa kike katika mtandao              wa facebook na kusema "Ningependa kuomba msamaha kwa              wanawake wote."
        
Comments
Post a Comment