TOTTENHAM HOTSPURS inatajwa kuwa tayari kuvunja rekodi            yao ya manunuzi kwa kutoa kitita cha paundi milioni 40 ili            kumsajili Isco kutoka Real Madrid Januari mwakani.
        Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 amekuwa akihangaika            kupata nafasi katika kikosi cha Zinedine Zidane, akianza            katika mechi mbili pekee msimu huu na alikuwa akihusishwa na            tetesi za kwenda Spurs kipindi cha kiangazi.
        Isco aliyenunuliwa na Madrid kutoka Malaga miaka mitatu            iliyopita tayari ameeleza nia yake ya kuondoka kama atakosa            nafasi katika kikosi cha kwanza.
        
Comments
Post a Comment