PEP Guardiola              ameponda staili ya Manchester United ya kutumia mipira              mirefu wakati akifafanua anachotaka kukiona kwa timu yake ya              Manchester City.
        City walilala 1-0              Old Trafford katika mechi ya EFL katikati ya wiki na              ikaelezwa kwa Guardiola kwamba timu yake ilishindwa kucheza              kwa staili yao kutokana na ukabaji wa kutumia kasi kubwa wa              United.
         Guardiola              hakulichukulia poa jambo hilo akisisitiza kwamba timu yake              inaweza kucheza soka mbele kwa mbele lakini kikosi cha Jose              Mourinho kimeshindwa kutokana na kupiga mipira mirefu juu,              staili ambayo yeye kamwe hataitumia.
        "Dhamira ya              United ilikuwa ni mpira mrefu. Ukipoteza mpira unapogombea              kwa hewani wanakufunga goli," alisema.
        "Wakati mwingine              unafungwa goli kwa sababu unalazimika kuanza kujenga              mashambulizi kama haya. Na wakati mwingine unapiga mipira              mirefu na unafungwa pia."
        
Comments
Post a Comment