MWIGIZAJI mkongwe              wa filamu, Abdallah Mkumbila "Muhogo Mchungu" anamsaka kwa              udi na uvumba mtu aliyemzushia kifo kwenye mitandao ya              kijamii ilihali yeye ni mzima wa afya tele.
        Alisema kuwa,              mitandao ya kijamii ni kama kisu, ukiitumia vibaya inaweza              kusababisha madhara makubwa katika jamii na kuwataka watu              waitumie vizuri ili wasilete madhara kwa jamii.
        "Sijui huyo              aliyezusha hayo mambo alikuwa na maana gani, kwani amezua              taharuki kwenye familia yangu na katika jamii. 
        Nataka kwenda              TCRA ili niweze kumjua nani amefanya hivyo ili tumfikishe              kwenye vyombo vya sheria," mwigizaji huyo alikiambia kipindi              cha "Super Mix" cha East Africa Radio.
        "Mimi ni mzima wa              afya njema kabisa sio marehemu kama watu wanavyosema, nipo              Bagamoyo na katika wiki mbili hizi sijasumbuliwa hata na              mafua, nimesikia hizo tarifa za kifo changu na nimetumiwa              mpaka picha."
        
Comments
Post a Comment