KIUNGO wa              Manchester City, Ilkay Gundogan ameiita Manchester United              timu isiyo na adabu kwa kitendo ilichomfanyia Mjerumani              mwenzake, Bastian Schweinsteiger.
        Schweinsteiger              alijiunga na Man United akitokea Bayern Munich majira ya              joto mwaka 2015 na amecheza mechi 31 katika msimu wake wa              kwanza katika soka la Uingereza.
        Mkongwe huyo, 32,              amekosa nafasi katika kikosi cha Jose Mourinho, hata hivyo              Gundogan amebwatuka kuwa mashetani wekundu hawajamtendea              haki mshindi huyo wa Kombe la Dunia.
        "Naamini kwamba              Manchester United inaweza kufaidika kwa asilimia 100 kutoka              kwa Bastian Schweinsteiger," Gundogan aliiambia Sport Bild.
        "Kama kila              tunachosikia na kusema ni kweli, naweza kusema wamemvunjia              heshima, yeye si mchezai yule wa awali, si Yule wa miaka 18              au 19."
        Klabu kadhaa              zimetajwa kuitamani huduma ya kiungo huyo mwenye uzoefu              mkubwa, ikiwa ni pamoja na MLS ya Galax ambayo ilionyesha              nia ya kumsajili mwishoni mwa mwezi uliopita.
        
Comments
Post a Comment