KABLA ya Ahamisi            usiku, Paul Pobga alikuwa sawa na gari la kifahari lilofungiwa            ndani. Lakini katika mchezo wa Europa League dhidi ya Fenerbahce, Mourinho akafungua geti na            kulitoa hadharani 'gari' na kuliendasha huku akiwakoga            majirani wenye wivu.
        Mchazaji huyo            ghali duniani kwa mara ya kwanza akaonyesha kile kilichofanya            Manchester United imsajili kwa pauni milioni 89.
        Pobga aling'ara            vilivyo katika mchezo huo wa Europa League na kuiwezesha            Manchester United kuibuka na ushindi wa bao 4-1 dhidi ya miamba hiyo ya Uturuki.
        Licha ya Pobga kuzunguka uwanja mzima na kusambaza            mipira kwa ustadi wa hali ya juu, lakini pia alifunga magoli            mawili, moja likija kwa mkwaju wa penalti na liingine            akiunganisha kwa umahiri pasi ya Lingard.
        Kiungo  alipiga pasi za            uhakia 78 ukilinganisha na 38 alizotoa katika mchezo dhidi ya            Liverpool Jumatatu usiku.
        Paul Pogba aling'wakati              ara  jana Manchester United ikiiadhibu Fenerbahce 
        Paul Pogba alitupia              magoli mawili
        Pogba akifunga bao la              kwanza kwa penalti
        
Comments
Post a Comment