KOCHA nguli              katika Ligi Kuu ya England, Harry Redknapp aliyezinoa timu              tano kwa nyakati tofauti, amefichua kuwa kuna upangaji              matokeo mkubwa katika Ligi hiyo.
        Alisema,              anafahamu kuwa kuna nyakati wachezaji wake walipanga matokeo              katika mechi walizocheza.
        Kwa nyakati              tofauti, Redknapp alipata kuzinoa Westham United,              Portsmouth, Southampton, Tottenham na Queens Park Rangers.
        Mbali na              Redknapp, pia mmoja wa viongozi wa soka Italia, Pino              Pagliara alikiri kufahamu uwepo wa upangaji matokeo katika              Ligi Kuu England.
        Kocha huyo              mkongwe alisema jukumu la kufanya uchunguzi huo halipaswi              kuachwa kwa FA pekee bali bodi ya FIFA ya kupambana na              rushwa michezoni.
        
Comments
Post a Comment