STAA Thomas              Muller anaonekana kukunwa na kiwango kilichoonyeshwa na timu              yake ya Bayern Munich usiku wa kuamkia jana katika michuano              ya Ligi ya Mabingwa na kuwawezesha kuondoka na ushindi wa              mabao 4-1 dhidi ya PSV.
        Katika mchezo huo              uliopigwa kwenye uwanja wa Allianz Arena, vijana hao wa              kocha Carlo Ancelotti waliingia dimbani wakiwa wameshatoka              kapa mara atu mfululizo bila kupata ushindi lakini wakaweza              kuzinduka na kuwatembezea kipigo Waholanzi hao.
        Alikuwa Muller              ambaye alifungulia mvua ya mabao kwa kupachika la kwanza              ikiwa ni la tatu msimu huu kabla ya nyota mwenye kiwango cha              hali ya juu, Joshua Kimmich kupachika la pili.
        Hata hivyo,              Luciano Narsiagh aliisawazishia PSV bao moja lakini Roberto              Rewandowsk na Arjen Roben wakaongeza mengine mawili baada ya              timu hizo kutoka mapumziko.
        "Tulianza na kasi              tangu dakika ya kwanza," Muller aliiambia tovuti ya klabu              hiyo.
        "Tulifanya              mashambulizi mengi hususan dakika 30 za kwanza. Ulikuwa ni              mchezo mzuri. Tulitaka kuonyesha kiwango kizuri tofauti na              ilivyokuwa katika mechi chache zilizopita. Bao la kwanza              lilikuwa muhimu kwa sababu tulikuwa tukijutia nafasi              tulizozipoteza mwanzo," aliongeza staa huyo.
        Kwa upande wake              Robben alisema kuwa anavyodhani Bayern walistahili kushinda              lakini alisema kuwa hakuweza kucheza katika ubora wao kwa              muda wote wa dakika 90.
        
Comments
Post a Comment