HAKUNA ubishi              Liverpool wazuri msimu huu acha kabisa. Wameanza vizuri              msimu na wanaendelea kupeta wanavyotaka.
        Hata hivyo pamoja              na ubora wao wote huo, bosi Jurgen Klopp amesema ubingwa              msimu huu kwa timu yake bado kabisa.
        Ni sawa na kauli              ya kukatisha tama, lakini kwa kocha huyo raia wa Ujerumani              anaona Ligi ndio kwanza mbichi na kuongelea ubingwa wa              kikosi chake ni sawa na kupoteza muda wakati huu.
        "Reds" ni moja ya              timu tatu za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu England,              inakusanya pointi 20 ikiwa nyuma ya Manchester City na              Arsenal kwa tofauti ya mabao. 
        Liverpool tayari              imeshacheza na vigogo kama Arsenal, Tottenham Hotspur,              Leicester, Chelsea na Manchester United katika mechi nane za              kwanza msimu huu, lakini Klopp anasema ni mapema sana              kufikiria ubingwa kwa sasa. 
        "Sijali. Ni              masuala ya kawaida kwenye soka timu inapofanya vizuri watu              wanaanza kuzungumzia nafasi ya ubingwa."
        "Sishawishiki              kuamini kila kinachozungumzwa na watu kuhusu sisi. Safari              bado ni ndefu na kwa sababu hiyo huwezi kuzungumzia masuala              ya ubingwa kwa sasa," alisema kocha huyo wakati akizungumza              na waandishi wa habari.
        
Comments
Post a Comment