DEMU AMPONZA MCHEZAJI NEW ZEALAND… apigwa marufuku kucheza mchezo mmoja baada ya kuingia nae msalani
MCHEZAJI wa timu              ya Raga ya New Zealand, Aaron Smith amepigwa marufuku              kucheza mchezo mmoja baada ya kuingia msalani na mwanamke              katika uwanja wa ndege mjini Christchurch.
        Hiyo ni kinyume              na kanuni za timu hiyo ya taifa.
        Atakosa mchezo wa              ubingwa wa Raga dhidi ya Afrika Kusini mjini Durban.
        Kocha wa All              Bracks, Steve Hansen amesema Smith mwenyewe amesikitishwa              sana na kitendo hicho.
        Hansen ameongeza              kwamba mchezaji huyo wa miaka 27 anahisi kwamba ameivunja              moyo timu yake, familia yake na mpenzi wake.
        "Ameomba kwenda              nyumbani kushughulikia masuala ya kibinafsi ambayo yameibuka              kutokana na kisa hicho na tuna furaha kumsaidia katika              hilo," amesema Hansen.
        Kocha huyo              amesema adhabu hiyo iliafikiwa na kundi la viongozi wa timu              ambalo lilijumuisha wachezaji.
        Smith amechezea              New Zealand mashindano 54 tangu aanze kuwachezea mwaka 2012.              Baadae mwaka 2012 alizuiwa kucheza kwa muda kwa kuvunja amri              ya kutotoka nje.
        Mwaka 2014              alituma picha yake ya utupu kwenye snapchat ambayo ilisambaa              sana mitandaoni.
        
Comments
Post a Comment