NYOTA wa Brazil,              Oscar dos Santos Emboaba Junior, bado ana maisha marefu ya              kuichezea klabu ya Chelsea baada ya kuonyesha uwezo wake wa              kuisaidia The Blues kupata ushindi katika mchezo wao wa              mwisho katika ziara nchini Marekani.
        Nyota huyo mwenye              umri wa miaka 24 alipachika mabao mawili na kuifanya Chelsea              kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Milan ikiwa ni              mwanzo mzuri wa kocha mpya, Antonio Conte na anafarijika              kuona timu yake inafanya vizuri katika mchezo dhidi ya Milan              ambayo ni timu nzuri.
        Hata hivyo,              Chelea iliwapa nafasi mastaa Diego Costa aliyekuwa majeruhi,              N'Golo Kante aliyeingia akitokea benchi na Eden Hazard              alipata nafasi ya kucheza dakika chache tu.
        Kinda wa Chelsea,              Bertrand Traore alifanikisha klabu yake kuongoza lakini              jitihada zake zilifelishwa na kiungo Muitaliano, Giacomo              Bonaventura, baada ya kusawazisha bao lake kwa kupiga moja              kwa moja mpira wa adhabu.
        Chelsea walikuwa              na hali ngumu baada ya washambuliaji wa AC ilan kufanya              mashambulizi ya mara kwa mara na kumpa kazi ya ziada              Azpilicueta licha ya umahiri wa mlinda mlango Thibaut              Courtois kulinda vizuri lango lake.
        Licha ya Mbrazil              Willian kudhibitiwa na Donnarumma, aliongezewa nguvu na              Fabregas kabla ya mlinda mlango wa Milan kuchukua maamuzi ya              kutoka ili kuokoa mpira ule.
        Lakini katika              kipindi cha pili, mabadiliko ya Oscar yalifanya matumanini              ya Conte kurudi baada ya kuongeza nguvu na kupachika mabao              mawili yaliyosababisha ushindi huo mnono.
        
Comments
Post a Comment