WENGER APANIA KUENDELEA KUMTUMIA WALCOTT KAMA MSHAMBULIAJI WA KATI


WENGER APANIA KUENDELEA KUMTUMIA WALCOTT KAMA MSHAMBULIAJI WA KATI
Arsene Wenger amedhamiria  kuendelea kumtumia Theo Walcott kama mshambiliaji wa kati licha ya mchezaji huyo kudai sasa anataka kubakia kama winga. 

Baada ya miaka mingi ya kumshawishi kocha wa Arsenal kwamba anaweza kucheza kama mshambuliaji, Walcott aligeuza mawazo wiki iliyopita kwa kusema anataka kutambulika kama winga wa kulia.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 alianza kama mshambuliaji wa kati katika mchezo wa ushindi wa bao 8-0 dhidi ya Vicking ya Norway siku ya Ijumaa na kufunga bao moja na kupika moja.
Arsenal manager Arsene                  Wenger has vowed to continue playing Theo Walcott as a                  striker
Kocha wa Arsenal  Arsene Wenger amesema ataendelea kumtumia Theo Walcott kama mshambuliaji
Since his arrival at the                  club in 2006, Walcott has suffered with a string of                  long-term injuries
Tangu asajiliwe Arsenal mwaka 2006, Walcott amekuwa akiumia mara kwa mara

REKODI YA THEO WALCOTT

Kuzaliwa: Machi 16, 1989
Timu: Southampton, Arsenal
Mechi alizocheza: 367
Magoli: 90
"Ninaamini Walcott ana vigezo vyote vya kuwa mshambuliaji mkubwa," alisema Wenger

"Amekuwa mzuri anapokimbia na mpira, ni mchezaji mwenye akili na mmaliziaji mzuri.

"Si mkabaji mzuri hivyo naamini kutumia mbio zake katika thelusi ya mwisho ya uwanja kutazaa matunda mazuri zaidi".






Comments