MSHAMBULIAJI              Sergio Aguero juzi alikosa penati mbili, moja ikipanguliwa              na kipa na nyingine ikienda nje, lakini akatuliza kichwa na              kufunga mabao matatu "hat trick" kuiwezesha Manchester City              kuibuka na ushindi wa mabao 5-0 nyumbani kwa Steaua              Bucharest nchini Romania.
        Ushindi huo              katika mchezo wa kwanza wa kufuzu hatua ya makundi ya Ligi              ya Mabingwa Ulaya umewaweka katika nafasi nzuri ya kufuzu              kwani wanahitaji sare yoyote watakaporudiana Agosti 24              nyumbani kwenye dimba la Etihad, mjini Manchester.
        Mabao mengine ya              City katika mchezo huo yalifungwa na David Silva na Nolito              ambapo kwa mara nyingine kocha Pep Guardiola alimchomesha              mahindi benchi kipa Joe Hart.
        Katika mchezo              mwingine wa mechi ya kufuzu, Borussia Monchengladbach ya              Ujerumani iliibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Young              Boys ya Uswisi.
        
Comments
Post a Comment