MANCHESTER UNITED YATWAA NGAO … IBRAHIMOVIC SHUJAA, JESSE LINGARD AFANYA VITU ADIMU


MANCHESTER UNITED YATWAA NGAO … IBRAHIMOVIC SHUJAA, JESSE LINGARD AFANYA VITU ADIMU

Ibrahimovic beats Leicester captain Wes Morgan to                  the ball in order to head home the winning goal

MSHAMBULIAJI mpya wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic ameipa timu hiyo taji la kwanza msimu huu baada ya kufunga bao la ushindi lililoipa United Ngao ya Hisani dhidi ya Leicester City.

Katika mechi hiyo iliyomalizika kwa United kushinda 2-1, Ibrahimovic akaruka juu na kuunganisha kwa kichwa krosi ya Antonio Valencia hadi wavuni kukiwa kumesalia saba za mchezo.

United walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 32 kupitia kwa mshambuliaji wake chipukizi Jesse Lingard aliyefunga bao bora la mechi kutokana na juhudi zake binafsi za kuuchambua msitu wa mabeki wa Leicester  kwa chenga tamu kabla ya kumtungua kipa Schmeichel.

Leicester City wakafunga bao lao kunako dakika ya 52 kupitia kwa mshambuliaji wake hatari Jamie Vardy kufuatia makosa ya kiungo Marouane Fellaini.

Manchester United (4-2-3-1): De Gea 6.5, Valencia 6.5, Bailly 7, Blind 7, Shaw 7 (Rojo 69), Carrick 6.5 (Herrera 61), Fellaini 6, Lingard 7.5 (Mata 63, Mkhitaryan 90+3), Ibrahimovic 6.5, Rooney 6 (Schneiderlin 88), Martial 6 (Rashford 70)

Leicester City (4-4-2): Schmeichel 6.5, Simpson 6.5 (Hernandez 63), Huth 6 (Ulloa 89), Morgan 5, Fuchs 6.5 (Schlupp 80), Mahrez 6, Drinkwater 7, King 6.5 (Mendy 63), Albrighton 6 (Gray 46), Okazaki 6 (Musa 46), Vardy 7

Manchester United's players celebrate with the                  Community Shield after beating Leicester 2-1 at Wembley                  Stadium
Wachezaji wa Manchester United na Ngao ya Hisani
Zlatan                  Ibrahimovic roars with delight after scoring a late                  winner for Manchester United in the Community Shield
Zlatan Ibrahimovic akishangilia goli lake
Ibrahimovic rose highest at the back post to beat                  Kasper Schmeichel and put United 2-1 up against                  Leicester
Ibrahimovic akishangilia na Mata na Rooney
Jesse                  Lingard (second right) slots past Leicester City                  goalkeeper Schmeichel to put Manchester United 1-0 up
Jesse Lingard (wa pili kushoto) akipiga mpira unaompita kipa wa Leicester na kuwa goli la kwanza kwa United
Lingard (centre) is joined by Manchester United                  captain Wayne Rooney in celebration after his opener
Lingard (katikati) na mbwembwe na kufurahia goli
Jamie                  Vardy levelled things up for the Premier League                  champions after taking the ball around David de Gea
Jamie Vardy anasawazisha
A                  horrific defensive error from Marouane Fellaini (left)                  gifted Vardy the chance to equalise for Leicester
Makosa ya ukabaji ya Marouane Fellaini (kushoto) yakatoa mwanya kwa Vardy kuisawazishia Leicester




Comments