KOCHA Claudio              Ranieri amesema hakuna nafasi ya Leicester kuporomoka katika              mbio zake za kutetea ubingwa wa Ligi Kuu England, kama              ilivyokuwa kwa Chelsea msimu uliopita.
        The Blues ilitwaa              ubingwa mwaka 2015 lakini ilikuwa na mwanzo mbaya mwaka              uliopita, hatua iliyosababisha kutimuliwa kwa kocha Jose              Mourinho, kabla ya timu hiyo kumaliza nafasi ya 10 katika              msimamo wa Ligi.
        Kwa namna ambavyo              Lesester ilifanikiwa kutwaa ubingwa ikiwa ni mwaka mmoja              baada ya kupigana kufa na kupona kujinasua kushuka daraja,              mabingwa hao ambao leo wanavaana na kikosi kipya cha              Mourinho, Manchester United kwenye Ngao ya Jamii kwenye              uwanja wa Wembley, wanaamini msingi waliojijengea              utawasaidia kutetea ubingwa wao.
        Ranieri anataka              makubwa zaidi msimu huu. "Wakati ninapojenga kitu fulani              kamwe hakibomoki," alisema kocha huyo mzoefu raia wa Italia.
        "Falsafa yangu ni              kutazama nyumba yangu si ya wengine. Ni muhimu kwa kile              kinachotokea hapa. Nyumba yangu ni safi sana na ipo wazi.              Taratibu tumejaribu kujenga ghorofa ya kwanza na ya pili.              Msingi ni imara sana."
        
Comments
Post a Comment