JOSE MOURINHO ASEMA ALICHOKIFANYA KWA SCHWEINSTEIGER SAHIHI ...adai panga ni lazima ili kupisha nyota wapya



JOSE MOURINHO ASEMA ALICHOKIFANYA KWA SCHWEINSTEIGER SAHIHI ...adai panga ni lazima ili kupisha nyota wapya
Jose Mourinho amejitetea juu ya uamuzi wake wa kumtosa kiungo mkongwe Bastian Schweinsteiger na kusisitiza kuwa anataka kufanyabkazi na wachezaji 23 Manchester United.

Mourinho amekuwa kikaangoni baada ya kumlazimisha Mjerumani huyo mshindi wa Kombe la Dunia kufanya mazoezi na kikosi cha chini miaka 23 (U-23). 

Kocha huyo mpya wa United amejitetea kuwa alichokifanya ni sahihi na kwamba anapaswa kupiga panga kikosi chake ili kupisha wachezaji wapya wanne aliowasajili hadi muda huu.
Jose Mourinho has defended                  his treatment of midfielder Bastian Schweinsteiger
Jose Mourinho amejitetea kwa kile alichomtendea Bastian Schweinsteiger
The Germany midfielder was                  banished to train with the reserve team last week
Kiungo mkongwe wa Ujerumani alilazimishwa kufanya mazoezi na kikosi cha pili wiki iliyopita

"Ninapaswa kufanya maamuzi yangu. Ni hivyo tu," alisema Mourinho alipoulizwa juu ya alichokifanya kwa Schweinsteiger.

"Kilichofanyika ndicho kinachofanyika katika kila klabu ulimwenguni, ni kocha ndiye anayeamua juu ya kikosi chake".



Comments