KOCHA wa Manchester City, Pep Guardiola              amewataka wachezaji kuwepo majumbani mwao na familia zao              siku moja kabla ya mechi, badala ya kukaa kwenye hotel au              viwanja vya mazoezi.
        Utaratibu huo unamfanya Guardiola              kuifanya Man City kuwa klabu ya kwanza ya Ligi Kuu England              kulala katika viwanja vya mazoezi tangu walipofungua City              Football Academy mwishoni mwa mwaka 2014.
        Awali Man City walikuwa wakikaa hotelini              karibu na viwanja vya mazoezi kama mahasimu wao, Manchester              United katika mechi wanazochezea nyumbani.
        Guardiola alisema: "Kama hawatapumzika              hawatakuwa makini siku ya mechi, hivyo watapoteza kazi zao              kwa kucheza vibaya. Mimi sio polisi ninawahukumu wachezaji              wangu kwa kazi wanayoifanya na sio maisha yao binafsi."
        
Comments
Post a Comment