TAARIFA kutoka              katika klabu ya Real Madrid zimedai kuwa staa wao, Cristiano              Ronaldo amekubali kuongeza mkataba utakaomfanya kubaki              klabuni hapo hadi mwaka 2020 au 2021.
        Imeelezwa kuwa              winga huyo wa kimataifa wa Ureno anajiandaa kukutana na              wakala wake, George Mendes na rais wa Madrid Florentino              Perez ili kukamilisha mchakato huo.
        Mshindi huyo mara              tatu wa Ballon d'Or alikuwa akitajwa kutimka Bernabeu, hasa              baada ya kutokuwa kwenye ubora wake katikati ya msimu              uliopita.
        Kwa mujibu wa              taarifa hizo, Ronaldo, Mendes na Perez watakutana Agosti 10              ikiwa ni baada ya nyota huyo kurejea kutoka mapumzikoni.
        
Comments
Post a Comment