ZLATAN IBRAHIMOVIC APEWA JEZI NAMBA 9 MANCHESTER UNITED …Paul Pogba abakiziwa namba 6, Anthony Martial mmmh!



ZLATAN IBRAHIMOVIC APEWA JEZI NAMBA 9 MANCHESTER UNITED …Paul Pogba abakiziwa namba 6, Anthony Martial mmmh!
Zlatan Ibrahimovic has not travelled to China with              Manchester United

Zlatan Ibrahimovic amekabidhiwa jezi namba 9 Manchester United huku aliyekuwa akiimiliki namba hiyo Anthony Martial akipewa jezi namba 11.

Mshambuliaji huyo wa Sweden amezitumikia jezi namba 8,9 na 1o katika maisha yake ya soka na ilitarajiwa kuwa angekumbana na namba tofauti na hizo tatu ndani ya Manchester United kutokana na ukweli kuwa tayari jezi hizo zilikuwa zinamilikiwa na wachezaji wengine.

Lakini sasa Martial anahamia jezi namba 11 wakati Adnan Januzaj  aliyekuwa akiitumikia namba hiyo, anapewa jezi namba 15. Juan Mata anabakia na namba 8 yake na Wayne Rooney anaendelea kuimiliki jezi namba 10.

Ibrahimovic ametupia picha ya jezi No 9 kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuandika: "Nimechagua namba 9." 

Wachezaji wengine wapya wa United Eric Bailly na Henrikh Mkhitaryan, wamechukua jezi namba 3 na 22. 

Jezi namba No 6 imeachwa wazi -haina mwenyewe - pengine imeachwa kwaajili Paul Pogba ambaye huwa anaivaa jezi hiyo katika klabu yake ya Juventus.
United's new signing                  Ibrahimovic posted this image on Instagram with the                  caption: 'I chose the number 9' 
Ibrahimovic ametupia picha ya jezi No 9 kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuandika: "Nimechagua namba 9." 
The provisional United squad                  numbers for the 2015-16 season, showing Ibrahimovic as                  No 9
Orodha mpya ya wachezaji wa Manchester United na namba zao za jezi




Comments