WAYNE ROONEY AINGIWA HOFU MAN UNITED



WAYNE ROONEY AINGIWA HOFU MAN UNITED

Wayne

Nahodha wa Manchester United Wayne Rooney amekiri kwamba yuko kwenye wakati mgumu baada ya klabu kuanza kuleta wachezaji wenye majina makubwa.

Hadi sasa United imeshakamilisha usajili wa wachezaji watatu Eric Bailly Henrikh Mkhitaryan na Zlatan Ibrahimovic huku kukiwa na kila dalili ya kumsajilia Pogba pia.

Kiongozi huyo wa wachezaji wa mashetani wekundu amesema anatakiwa kuwa kwenye kiwango bora ili kuendelea kulinda nafasi yak echini ya kocha mpya Jose Mourinho.

"Wakati wote unatakiwa kuthibitisha ubora wako katika kila msimu, kwasababu ni ndoto ya kila mchezaji kupata nafasi ya kucheza. Nadhani unakuwa na furaha ukiwa unacheza kwenye kikosi cha Manchester United."



Comments