UJERUMANI imekosa penalti tatu katika hatua ya mikwaju ya penalti kwenye mchezeo wa robo fainali dhidi ya Italia, lakini bado wakashinda na kutinga nusu fainali ya Euro 2016.
Timu hizo zilikwenda sare ya 1-1 ndani ya dakika 120 na ilipofika hatua ya mikwaju ya penalti Ujerumani wakashinda 6-5.
Miamba hiyo ya soka barani Ulaya ililazimika kwenda hadi penalti ya tisa ndipo mshindi alipopatikana kwa Italia kupoteza jumla ya penalti nne huku Ujerumani wakipoteza tatu.
Ujerumani walipata bao la kuongoza dakika ya 65 kupitia kwa Mesut Ozil lakini Leonardo Bonucci akaisawazishia Italia kwa njia ya penalti dakika ya 78.
Hivi ndivyo penalti zilivyopigwa
Jonas Hector akishangilia penalti yake iliyoipa Ujerumani ushindi dhidi ya Italia
Hector akishangiliwa na wenzake
Italia hoi
Matteo Darmian akikosa penalti
Comments
Post a Comment