STRAIKA wa timu              ya taifa ya Ujerumani, Thomas Muller ameweka wazi kwamba              hataweza kupiga tena penati, baada ya majuzi kushindwa              kuziona nyavu katika mechi ya robo fainali ya michuano ya              fainali za mataifa ya Ulaya "Euro 2016" ambayo waliibuka na              ushindi dhidi ya Italia.
        Katika mchezo huo              uliopigwa Jumapili usiku, mabingwa hao wa dunia walikuwa              wakihitaji ushindi wa penati baada ya kwenda sare ya bao 1-1              na Italia katika muda wa dakika 120, lakini Muller ni mmoja              kati ya nyota watatu wa Ujerumani waliokosa kuziona nyavu              wakiwa yadi 12, baada ya shuti lake kuokolewa na mlinda              mlango Gianluig Buffon.
        Straika huyo              mahiri vilevile aliwahi kuikosa penati wakati wa mechi ya              Bayern Munich dhidi ya Atletico Madrid katika mechi ya nusu              fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa na sasa anaonekana              kuamua kutopiga tena mipira hiyo.
        "Sitapiga tena              penati katika kipindi cha wiki mbili zijazo," Muller              aliliambia jarida la Sport Bild.
        "Nitajifunza              mwenyewe kutafuta mbinu za kufunga penati na nitarejea              nikiwa fiti katika kipindi vcha mwezi mmoja ama miwili,"              aliongeza.
        
Comments
Post a Comment