STRAIKA Michy              Batshuayi yuko mbioni kutua katika klabu ya Chelsea baada ya              kufuzu vipimo vya afya jijini Bordeaux, kwa mtandao wa Sky              Sports.
        Batshuayi aliye              kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ubelgiji kwenye michuano              ya mataifa ya Ulaya "Euro 2016", amekuwa akihusishwa na              klabu kubwa Ulaya baada ya kufunga mabao 17 akiwa Marseille              msimu uliopita.
        Mshambuliaji huyo              alipewa ruhusa kufanya vipimo na kocha wake katika timu ya              taifa kwa ajili ya kukutana na timu ya madaktari wa Chelsea              kwa ajili ya kukamilisha uhamisho utakaogharimu pauni mil              33.
        
Comments
Post a Comment