Sentahafu              wa Ureno Pepe amerejea katika mazoezi kamili kujiandaa na              mchezo wa fainali ya Euro 2016  dhidi ya wenyeji Ufaransa              utakaochezwa Jumapili.
        Pepe              ambaye pia ni sentahafu wa Real Madrid aliukosa mchezo wa              ushindi wa 2-0 katika nusu fainali dhidi ya Wales baada ya              kuumia paja kwenye mechi ya robo fainali iliyowakutanisha na              Poland.
          Beki              huyo alifanya mazoezi ya peke yake Alhamisi na Ijumaa lakini              Jumamosi akaungana na wachezaji wenzake kufanya mazoezi ya              pamoja na sasa anatarajiwa kuanza katika mtanange wa              fainali.
          Nahodha              wa Ureno Cristiano Ronaldo ameweka wazi kuwa amefurahishwa              na kurejea kwa Pepe na kusema anaamini beki huyo kisiki              atachagiza ushindi siku ya Jumapili.
        Sentahafu                wa Real Madrid Pepe amerejea kundini
          Nahodha                wa Ureno Cristiano Ronaldo anaamini Pepe atachagiza                ushindi katika mchezo wa fainali dhidi ya Ufaransa
          
Comments
Post a Comment