RONALDO AFURAHIA KUREJEA UWANJANI KWA PEPE



RONALDO AFURAHIA KUREJEA UWANJANI KWA PEPE
Sentahafu wa Ureno Pepe amerejea katika mazoezi kamili kujiandaa na mchezo wa fainali ya Euro 2016  dhidi ya wenyeji Ufaransa utakaochezwa Jumapili.

Pepe ambaye pia ni sentahafu wa Real Madrid aliukosa mchezo wa ushindi wa 2-0 katika nusu fainali dhidi ya Wales baada ya kuumia paja kwenye mechi ya robo fainali iliyowakutanisha na Poland.

Beki huyo alifanya mazoezi ya peke yake Alhamisi na Ijumaa lakini Jumamosi akaungana na wachezaji wenzake kufanya mazoezi ya pamoja na sasa anatarajiwa kuanza katika mtanange wa fainali.

Nahodha wa Ureno Cristiano Ronaldo ameweka wazi kuwa amefurahishwa na kurejea kwa Pepe na kusema anaamini beki huyo kisiki atachagiza ushindi siku ya Jumapili.
Real Madrid defender Pepe                    is back in contention for Portugal after recovering                    from a thigh injury
Sentahafu wa Real Madrid Pepe amerejea kundini
Portugal captain Cristiano                    Ronaldo believes the team can deliver the nation's                    first-ever major titleĀ 
Nahodha wa Ureno Cristiano Ronaldo anaamini Pepe atachagiza ushindi katika mchezo wa fainali dhidi ya Ufaransa


Comments