STRAIKA Radamel              Falcao amefanikiwa kufunga bao lake la kwanza tangu              aliporejea Monaco, lakini bao hilo halikuwazuia kuambulia              kupata kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Fenerbahce.
        Baada ya              kushindwa kupata mafanikio wakati akikipiga kwa mkopo katika              timu za Manchester United na Chelsea, Falcao ameamua kurejea              kwa vinara hao wa Ligue 1 ambapo mkataba wake bado una miaka              miwili.
        Katika mchezo huo              wa usiku wa kuamkia jana ulipogwa kwenye uwanja wa Sukuru              Saaracogru, staa huyo mwenye umri wa miaka 30 alipangwa              kikosi cha kwanza katika safu ya ushambuliaji na akaweza              kuyatumia vizuri makosa yaliyofanywa na mabeki wa timu              pinzani.
        Bao hilo la              kipindi cha kwanza cha Falcao lilifungwa na mchezaji              Emmanuel Emenike, lakini kwa mara nyingine tena staa huyo wa              zamani wa timu ya Westham akaihakikishia ushindi timu yake              kutoka Uturuki.
        
Comments
Post a Comment