Arsenal inakaribia            kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Japan Takuma Asano baada kufikia makubaliano na klabu yake            ya Sanfrecce Hiroshima.
        Takuma Asano            mwenye umri wa miaka 21 anakwenda Emirates na kufanya idadi ya            wachezaji wa Kijapan kutumikia Arsenal kufikia watatu baada            ya  Junichi Inamoto na Ryo            Miyaichi.
        Klabu kadhaa            zilikuwa zikiwania saini ya Asano lakini Arsenal imeshinda            vita baada ya kufikia makubaliano na klabu ya Sanfrecce Hiroshima.
        Mshambuliaji huyo            aliyeichezea Japan mechi nne na kuifungia bao moja,            anachukuliwa kama hazina ya baadae ya Arsenal na huenda            akatolewa kwa mkopo msimu ujao.
        Arsenal imekubali dili              la kumsajili nyota wa kimataifa wa Japan Takuma Asano kutoka              Sanfrecce Hiroshima
        Mshambuliaji huyu              anachukuliwa kama moja ya hazina ya kocha Arsene Wenger na              anaweza kutolewa kwa mkopo msimu ujao.
        
Comments
Post a Comment