MANCHESTER UNITED YAMTIA MKONONI HENRIKH MKHITARYAN WA BORUSSIA DORTMUND



MANCHESTER UNITED YAMTIA MKONONI HENRIKH MKHITARYAN WA BORUSSIA DORTMUND

Manchester United ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha usajili wa kiungo mchezeshaji wa Borussia Dortmund  Henrikh Mkhitaryan.

Borussia Dortmund imefichua kupitia mtandao wao rasmi kuwa kiungo huyo anaondoka na wanamtakia kila la kheri.

Klabu hiyo imesema haikuwa na namna nyingine zaidi ya kumuuza  Mkhitaryan kwa kuhofia kumpoteza bure msimu ujao.

"Borussia Dortmund na kiungo  Henrikh Mkhitaryan (27) wanaachana rasmi kiangazi hiki," alisema mtendaji mkuu wa klabu hiyo  Hans-Joachim Watzke.

Nahodha huyo wa kimataifa wa  Armenia ataungana na Zlatan Ibrahimovic ndani ya Old Trafford na kuwa usajili wa tatu wa  Jose Mourinho kiangazi hiki.

United inatarajiwa kulipa pauni milioni 26 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 ambaye amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake Borussia Dortmund.

Mkhitaryan ambaye bado hajakifikia makubaliano kuhusu maslahi yake binafsi na Manchester United, atahitajika kufuzu vipimo vya afya kabla usajili wake haujathibitishwa rasmi.

Pia atahitaji kupata kibali cha kufanya kazi England kabla dirisha la usajili la Premier League halijafungwa.

Borussia Dortmund ace                  Henrikh Mkhitaryan has completed his summer move to                  Manchester United
Nyota wa Borussia Dortmund  Henrikh Mkhitaryan amekamilisha usajili wa kujiunga na Manchester United
The Armenia international                    has swapped Borussia Dortmund for Manchester in a deal                    worth £26million
Borussia Dortmund imemuuza Henrikh Mkhitaryan kwa pauni milioni 26 kwenda Manchester United


Comments