KOCHA VECENTE DE BOSGUE AKIRI KUWA NA BIFU NA CASILLAS



KOCHA VECENTE DE BOSGUE AKIRI KUWA NA BIFU NA CASILLAS
KOCHA aliyeondoka katika kikosi cha timu ya taifa ya Hispania, Vecente Del Bosque amesema kwamba alituma ujumbe kwa kila mchezaji wake ili kueleza kuondoka kwake baada ya kutolewa katika fainali za Mataifa ya Ulaya "Euro 2016" isipokuwa mlinda mlango wao, Iker Casillas.

Juzi Del Busque alitangaza kuachia ngazi baada ya kushuhudia Hispania ikivuliwa ubingwa wa Ulaya na Italia katika hatua ya 16 Bora.

Katika kipindi cha miaka saba aliyokinoa kikosi hicho, kocha huyo mwenye umri wa  miaka 65, alishatwaa ubingwa wa Kombe la Dunia mwaka 2010 na fainali za mataifa ya Ulaya "Euro 2012".

Hata hivyo, Del Bousque alisema kuwa uhusiano wake na Casillas kwa sasa sio mzuri kutokana na kwamba mlinda mlango huyo anajisikia kutokuwa na furaha kutokana na kuwa hataki kuanzia benchi nyuma ya David de Gea.

"Kwa wachezaji wake anawasiliana nao vizuri, lakini kwa upande wa benchi la ufundi ni balaa," Del Bousque aliliambia jarida la El Larguero.


"Na hii ndio maana sikutuma ujumbe kwa Cassillas. Anajisikia vibaya kwangu mimi na si kwangu mimi tu hata kwa kocha wa viungo, Javier Minano, kocha msaidizi, Toni Grande. Kwa wengine hana shida lakini hasira zake ni kwetu," aliongeza kocha huyo.


Comments