KOCHA POCHETTINO ATHIBITISHA KUWATEMA NYOTA WATATU TOTTENHAM



KOCHA POCHETTINO ATHIBITISHA KUWATEMA NYOTA WATATU TOTTENHAM
KOCHA Mauricio Pochettino amethibitisha kwamba wachezaji Federico Fazio, Nabil Bentaleb na Alex Pirtichard msimu huu wasitarajie kuwa sehemu ya kikosi chake cha Tottenham.

Nyota hao watatu wameachwa kwenye kikosi hicho na Spur ambacho wiki hii kitacheza mechi za Kombe la mabingwa wa kimataifa dhidi ya timu za Juventus na Atletico Madrid sambamba na straika Clinton N'jie ambaye anahusishwa kutimkia katika timu ya Marseille.

Hata hivyo Pochettino anadai kuwa N'jie ameachwa jijini London kutokana na kuwa ni majeruhi, lakini inaonyesha Fazio, Bentaleb na Pritchard huenda wako katika mchakato wa kusaka timu mpya.

"N'jie ni majeruhi yupo jijini London na hawezi kucheza," alisema majuzi kocha huyo.


"Hali ya wachezaji wengine ipo wazi. Hawapo kwenye mipango yangu," aliongeza kocha huyo.


Comments