KOCHA wa              Liverpool, Jurgen Klopp ametaja kilichomfanya kumrejesha              nyumbani nyota wake Mamadou Sakho katika ziara yake nchini              Marekani.
        Amesema kwamba              bado ana mazungumzo ya kina na nyota huyo ambaye alikuwa              amefungiwa kwa matumizi ya dawa zisizoruhusiwa michezoni              kutokana na kuwa ameshafanya makosa mara tatu tangu amalize              adhabu hiyo.
        Akizungumza juzi              Mjerumani huyo alisema kwamba tangu nyota huyo afutiwe              mashitaka, ameshafanya makosa kadhaa na hivyo anahitaji              kukaa nae ili aweze kunusuru kibarua chake.
        "Hivi karibuni              kidogo akose ndege wakati Liverpool tukiondoka kwenda San              Francisco, alikuwa haji mazoezini na amekuwa akichelewa              kwenye chakula cha wachezaji," alisema Klopp.
        "Kwa hapa najenga              timu mpya na mwanzo wetu ni hapa. Nadhani italeta maana kama              aakirejea nyumbani Liverpool," aliongeza kocha huyo.
        Alisema kwamba              katika timu hiyo wana kanuni na sheria ambazo zinatakiwa              kuheshimiwa na kwamba kama kuna mtu ambaye hataki              kuziheshimu atamchukulia hatua.
        
Comments
Post a Comment