STAA mpya wa Liverpool, Joel Matip,              amesema kwamba kutokana na michuano ya Ligi Kuu England,              inataka mchezaji awe fiti, kwa hiyo mpango wake ni kwenda              kujifua gym kabla ya msimu huu mpya kuanza.
        Beki huyo mpya wa kati ambaye amejiunga              na klabu hiyo ya anfield akitokea Schalke, amesema juzi              kwamba bado kuna mambo mengi ya kufanya katika mwili wake              ili kuuweka sawa kabla ya Ligi hiyo kuanza.
        Mbali na kujifua gym kwa ajili ya Ligi              hiyo itakayoanza kutimua vumbi Agosti 13, mwaka huu, matip              mwenye umri wa miaka 24, pia mipango yake mingine ni              kuhakikisha anafikia kiwango cha hali ya juu.
        "Nipo tayari kwa ajili ya soka la              Uingereza, lakini kuna mambo mengi ya kufanya katika mwili              wangu," staa huyo aliiambia tovuti ya klabu katika siku yake              ya kwanza ya mazoezi ya kujiandaa na msimu ujao.
        "Hii ni Ligi tofauti hivyo ni lazima kuna              kitu cha kufanya katika mwili wangu ili niweze kiucheza              mahali hapa na ukiwa ni mwili wenye nguvu inatosha kucheza              katika Ligi hii," aliongeza staa huyo.
        
Comments
Post a Comment