HATIMAYE Zlatan Ibrahimovic amethibitisha kuwa anajiunga na Manchester United.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 34 amethibitisha hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo alisema sasa umefika wakati wa dunia kujua wapi anapoelekea na kufafanua kwa kusema: "Timu yangu ijayo ni Manchester United, nakuja".
Usajili wa Ibrahimovic wa kujiunga na Manchester United unategemewa kukamilika wikiendi hii.
Zlatan Ibrahimovic ameweka hadharani kuwa anajiunga na Manchester United
Ibrahimovic hakung'ara katika Euro 2016 akiwa na Sweden iliyotolewa katika hatua ya makundi
Ibrahimovic anaungana tena na Jose Mourinho (kulia) na atacheza dhidi ya kocha wake mwingine wa zamani enzi zake za Barcelona manager Pep Guardiola (katikati). Picha hii ya watatu hawa ilipigwa katika mchezo wa nusu fainali ya are Champions League ya mwaka 2010 kati ya Barcelona na Inter Milan
Namna Ibrahimovic atakavyoonekana katika jezi ya United msimu ujao

Comments
Post a Comment